Mahitaji

  • Mchele ½ kilo
  • Binzano ya njano kijiko 1 kikubwa
  • Vitunguu maji 2
  • Binzari nyembamba kijiko 1 chai
  • Iliki kijiko 1 kikubwa, twanga ½ na nyingine weka ikiwa nzima
  • Gram masala ½ kijiko cha chai
  • Mafuta vijiko 3 vikubwa
  • Hing kijiko 1 kidogo
  • Chumvi kijiko 1 kidogo
  • Mdalasini kijiko 1 kidogo
  • Tangawizi ya unga kijiko 1 kidogo

Maelekezo

Chakula rahisi kuandaa na chenye utamu wa kipekee. Unaweza kuongeza viungo unavyopenda ili kuongeza ladha ya chakula.

misosi-wali-bizari-main2

  • Andaa viungo – menya na vitunguu.
  • Weka mafuta yakipata moto, weka kitunguu maji. Angalia kisiive sana, kisha weka viungo vyote na koroga vizuri. Baada ya dakika 2, weka mchele na chumvi kisha koroga.
  • Weka maji ya moto kiasi funika, hakikisha mvuke hautoki. Punguza moto uwe mdogo sana.
  • Baada ya dakika 15, funua chakula, geuza na onja kama wali wa chini umeanza kuiva au umeiva kabisa. Ukiwa umeiva weka vijiko 3 vya maji, funika. Baada ya muda geuza.
  • Baada ya dakika 5 unaweza kuepua na kujiramba.

Unaweza kula chakula hiki mchana au usiku. Ni chakula muafaka kwa familia, lakini punguza viungo vikali kama kuna watoto wadogo wanaokula pia hiki chakula.

misosi-wali-bizari-main