Mahitaji
Fish fillet (steki ya samaki isiyokuwa na mifupa) kipande 1 kikubwa
Viazi (potato) 6 vya wastani
Kitunguu (onion) 1 kikubwa
Tangawizi na swaum (garlic and ginger paste) 1 kijiko cha cha chai
Breadcrumbs kiasi
Mayai (eggs) 2
Limao (lemon) 1/2
Chumvi (salt) kiasi
Pilipili (scotch bonnet chilli) 1/4
Curry powder 1/2 cha chai
Coriander powder 1/4 kijiko cha chai
Turmaric 1/4 kijiko cha chai
Fresh chopped coriander kiasi.
Mafuta ya kukaangia
Matayarisho
Chemsha viazi na chumvi kidogo kisha viponde na uviweke pembeni vipoe.Katakata
samaki vipande kisha mtie kwenye sufuria pamoja na tangawizi, swaum, limao na
chumvi. Mchemshe kidogo(hakikisha maji yote yanakauka) kisha mponde na uma
(folk) baada ya hapo tia spice zote,pilipili na vitunguu vilivyokatwa
vidogovidogo na uvipike pamoja na samaki kwa muda wa dk 3. Baada ya hapo tia
coriander na kamulia limao kisha viweke pembeni. Baada ya hapo changanya viazi
pamoja na mchanganyiko wa samaki kisha tengeneza maduara ya wastani. Baada ya
hapo piga mayai ktk bakuli na chumvi kidogo.Bandika jikoni mafuta ya
kukaangia ktk fry pan yawe kidogo tu (shallow fry) yakisha pata moto kiasi chukua
madonge yako kisha yachovye ktk mayai na umalizie ktk breadcrumbs kisha
zikaange ktk mafuta. Baada ya hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa
0 Comments
Post a Comment