Mahitaji

  • Nyanya
  • Pilipili hoho
  • Vitunguu maji
  • Vitunguuswaumu
  • Carrots
  • Ndimu
  • Nazi (tui zito)
  • Chumvi
  • Samaki
  • Tangawizi

Maelekezo

  • Andaa viungo – tangawizi, ndimu, vitunguu saumu – menya, kata na ponda kama inawezekana.
  • Osha samaki vizuri kisha mloweke kwenye viungo (chaganya tangawizi,ndimu,vitunguu saumu na chumvi) kwa muda wa saa moja.
  • Andaa viungo vyako mbadala – nyanya,vitunguu,karoti, na pilipili hoho. Tengeneza tui zito la nazi na hifadhi pembeni.
  • Bandika kikaangio, au sufuria jikoni, weka mafuta ya kula na acha yapate moto.
  • Weka samaki. Kaanga samaki ila hakikisha asikauke sana.
  • Fanya hivyo kwa samaki wote waliobaki.
  • Bandika sufuria jikoni weka mafuta kiasi – unaweza pia kutumia uliyokaangia samaki
  • Mafuta yakipata moto, weka vitunguu maji kisha koroga hadi kibadilike rangi kiwe rangi ya udongo.
  • Weka kitunguu saumu kisha koroga kidogo kama dakika 1
  • Weka pilipili hoho na karoti. Koroga kiasi, kwa takribani dakika 2.
  • Weka nyanya, koroga kiasi ili zichanganyike vizuri. Funika na mfuniko na acha ziive kwa mvuke.
  • Nyanya zikiiva, weka tui zito liache lichemke kama dakika 10.Mchuzi ukiwa mzito weka samaki na koroga mpaka samaki achanganyikane na viungo vizuri. Acha jikoni kwa dakika takribani 3 nakisha ipua.
  • Hapo msosi utakua tayari